Mshambuliaji
wa Barcelona, Luis Suarez (kushoto) akiwekeana mkwara na Sergio Ramos
wa Real Madrid (kulia) wakati wa mechi ya La Liga baina ya mahasimu hao
wa Hispania, maarufu kama El Clasico timu hizo zikitoa sare ya 2-2 usiku
wa Jumapili. Mabao ya Barca iliyomaliza pungufu baada ya Sergi Roberto
kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45 na ushei yalifungwa na Luis
Suarez dakika ya 10 na Lionel Messi dakika ya 52, wakati ya Real
yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya14 na Gareth Bale dakika ya 72. Ronaldo alitolewa anachechemea na nafasi yake kuchukuliwa na Marco Asensio dakika ya 46 baada ya kuumia enka
KOCHA WA ZAMANI WA YANGA, JACK CHAMANGWANA AFARIKI DUNIA MALAWI AKIWA ANA UMRI WA MIAKA 61
KOCHA wa zamani wa klabu ya Yanga SC, Jack Lloyd ‘Africa’ Chamangwana amefariki dunia asubuhi ya leo katika hospitali ya Queen Elizabeth Central (QECH) mjini Blantyre akiwa ana umri wa miaka 61. Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Malawi amefariki akiwa shujaa wa taifa lake na gwiji wa soka ya nchi yake pia mwenye heshima kubwa. Hadi anakutwa na umauti, Chamangwana alikuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Be Forward Wanderers na alikuwa kocha mkuu wa Nomads hapo kabla. Baada ya kuichezea The Flames mechi 133 akiwa na Nahodha pia na kuwemo kwenye kikosi kilichobeba Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mwaka 1978- 1979, Chamangwana akawa Kocha wa Malawi na Mkurugenzi wa Ufundi. Jack Chamangwana (kushoto) amefariki dunia asubuhi ya leo katika hospitali ya Queen Elizabeth Central (mjini Blantyre Mara ya mwisho alikuwa Kocha Msaidizi wa timu hiyo chini ya Young Chimodzi hadi Juni 2015 walipoondolewa na Chama cha Soka Malawi (FAM). ...

Maoni
Chapisha Maoni